Taarifa za wanahabari waliovuma kugeuka omba omba baada ya kufutwa ghafla kutoka vyombo vya habari zimekuwa zikishamiri.
Hilo linaonekana kuwafungua macho wenzao waliobahatika kubaki kazini na wengi wameingilia biashara za kutafuta mapeni zaidi.
Habari Nyingine: Serikali yaruhusu pombe kuuzwa kwenye lojigi

Mtangazaji mcheshi wa runinga ya KTN Zubeidah Koome ni mmoja wa wale ambao wanapanga safari yao ya kesho watakapoondoka kazini.
Jumatano Agosti 5 Koome aliwaonyesha mashabiki wake mradi wake ambao ameanza kuekeza katika kaunti ya Kajiado.
Habari Nyingine: Watu 48 wa familia ya mwanasiasa wapatwa na coronavirus, mmoja wao alisafiri kutoka Nairobi

Kwenye picha alizochapisha mtandaoni, Koome alionekana akiwa na wajenzi waliokuwa wakiendeleza kazi kwenye kipande cha ardhi.
Alisema anafuraha kuanza maisha ya uekezaji na kuomba Mwenyezi Mungu kumuongoza katika hilo.
Habari Nyingine: Jumatano Agosti 5: Watu 671 zaidi waambukizwa coronavirus
" Hauwezi kuweka muda kwa sababu ya matumizi ya kesho. Lakini unaweza kuwekeza kwa sababu ya kesho. Nimechangamka sana kwa sababu ya mradi wangu," aliwaambia mashabiki wake.
Wenzake akiwamo mtangazaji Masawi Japani walimkaribisha katika kaunti ya Kajiado ambapo watakuwa majirani.
Mtanagzaji mwenza Mary Kilobi, ambaye ni kipusa wake Francis Atwoli, pia ni mkazi wa Kajiado ambapo wana kasri lao.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjbH90fphmsa6alZ6xorSMpKaopZViurWtzaCYs5mannqiu82ynKygkWK6qr7AnaBmsZGgsm7FwGairqyRm8K1rYypnKyZXa%2BuqrDIZ5%2BtpZw%3D